Saturday, 15 November 2014




Kamanda wa UVCCM Wilaya Iringa mjini na Mjumbe wa Mkutano Mkuu wa Taifa wa CCM, Frederick Mwakalebela (kushoto)  amekabidhi vifaa vya muziki vyenye thamani ya shilingi milioni nane (8m/-) kwa Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Iringa mjini Abedi Kiponza (wa pili kushoto) na Katibu wa CCM Zongo Lobo Zongo (wa pili kulia) kwa ajili ya kusaidia shughuli za chama katika masuala ya kunadi sera na ilani ya uchaguzi ya mwaka  2010. Shughuli hiyo ilikwenda sambamba na kumuaga aliyekuwa mkuu wa mkoa wa iringa Dkt. Christine Ishengoma kichama ngazi ya wilaya.

BAADA ya kuachwa katika uteuzi wa  wakuu wa mikoa ,alisekuwa  mkuu  wa mkoa wa Iringa Dr Christine Ishengoma (pichani)amewaaga wakazi wa mkoa wa Iringa kwa  kuchangia kiasi cha Tsh milioni 19 kwa ajili ya kutekeleza agizo la Rais Jakaya Kikwete la ujenzi wa maabara katika  shule za  sekondari.
 Dr Ishengoma akifungua moja kati ya  vikao  vya RCC Iringa kulia ni mkuu wa wilaya ya Iringa Dr Leticia Warioba 

Akizungumza katika mahojiano maalum na mtandao  wa www.matukiodaima.co.tz  leo , Dr Ishengoma  ambae ni mbunge wa  viti maalum mkoa wa Morogoro (CCM)  alisema  kuwa pamoja na  kutemwa katika nafasi hiyo ya  ukuu wa mkoa ila bado anampongeza sana Rais Profesa Jakaya  Kikwete kwa uteuzi  wake kama mkuu  wa mkoa nafasi   iliyoishi  mapema  mwezi  huu baada ya rais kuteua wakuu wa mikoa wapya  wanne na kufanya mabadiliko kwa maadhi ya  wakuu wa mikoa nchini na Iringa nafasi yake kuteuliwa Bi Amina Juma Masenza .

Friday, 14 November 2014

Muziki wa dansi katika nchi za Afrika mashariki katika miaka ya hivi karibuni umeonekana kuzorota,wanamuziki wa zamani walikuwa na uwezo wa kupiga vyombo takribani vyote vya ala za muziki hali ni tofauti kwa sasa.
Tungo za zamani pia zilitokana na midundo asilia.
Leonard Mubali amefanya mahojiano na Hamza Kalala mwanamzuki mkongwe toka nchini Tanzania ambaye anauwezo wa kupiga vyombo vingi vya muziki na ambaye anauelezea muziki wa dansi wa sasa..CHANZO:BBC
 Rais wa Urusi Vladmir Putin amesema Marekani na
Umoja wa Ulaya, EU hautaathiri Urusi tu pekee isipokua uchumi wa dunia.
Putin amesema vikwazo hivyo vinakwenda kinyume na makubaliano ya kibiashara na kusema kuwa Umoja wa mataifa ndio ina haki kuweka vikwazo hivyo.
Vikwazo viliwekwa dhidi ya Urusi baada ya kuunga mkono kujitenga kwa jimbo la crimea lililokua sehemu ya Ukraine na kutuhumiwa kusaidia waaasi mashariki mwa nchi hiyo.
Putin ametoa kauli yake mjini Brisbane, Australia wakati huu wanapoelekea kwenye mkutano wa G20.
Viongozi wa dunia wakiwemo Putin, Rais wa Marekani,Barack Obama na Rais wa China,Xi Jinping wanakutana kwa siku mbili nchini Australia.

Thursday, 13 November 2014















































13 Novemba 2014 Imebadilishwa mwisho saa 16:17 GMT
Shirika la ndege la Kenya, Kenya Airways linasema limepata hasara ya dola milioni 116 katika kipindi cha nusu mwaka kinachomalizika mwezi huu wa Novemba.
Shirika hilo linasema hasara hiyo imetokana na mlipuko wa Ebola katika nchi tatu za Afrika Magharibi na kuzorota kwa hali ya usalama.
Mwandishi wa BBC aliyefuatilia taarifa hiyo Emmanuel Igunza anasema kuwa huu ni mwaka wa pili kwa kampuni hiyo kurekodi hasara. Idadi ya wasafiri imepungua mwaka huu kutokana na taarifa kuhusu hali mbaya ya usalama nchini Kenya.
Uhusiano kati ya mchezaji wa kimataifa wa Ujerumani na Arsenal Mesut Ozil na Baba yake Mustafa Ozil huenda ukawa umesambaratika kutokana na mabishano ya kisheria.
Mustafa aliifikisha kampuni ya masoko ya mwanaye mahakamani akidai pauni 495,000 za mapato yaliyopotea kwenye mkataba wa udhamini huku Mesut naye akidai kurejeshewa mkopo wake wa pauni 800,000
kesi hiyo mwishowe ilifikia tamati nje ya mahakama mwezi uliopita, lakini Mahakama imethibitisha hatua hiyo wiki hii.

Design by Victor Simon -