Rais wa Urusi Vladmir Putin amesema Marekani na
Umoja wa Ulaya, EU hautaathiri Urusi tu pekee isipokua uchumi wa dunia.
Putin amesema vikwazo hivyo vinakwenda kinyume na makubaliano ya kibiashara na kusema kuwa Umoja wa mataifa ndio ina haki kuweka vikwazo hivyo.
Vikwazo viliwekwa dhidi ya Urusi baada ya kuunga mkono kujitenga kwa jimbo la crimea lililokua sehemu ya Ukraine na kutuhumiwa kusaidia waaasi mashariki mwa nchi hiyo.
Putin ametoa kauli yake mjini Brisbane, Australia wakati huu wanapoelekea kwenye mkutano wa G20.
Viongozi wa dunia wakiwemo Putin, Rais wa Marekani,Barack Obama na Rais wa China,Xi Jinping wanakutana kwa siku mbili nchini Australia.

0 comments:
Post a Comment