Saturday, 15 November 2014

BAADA ya kuachwa katika uteuzi wa  wakuu wa mikoa ,alisekuwa  mkuu  wa mkoa wa Iringa Dr Christine Ishengoma (pichani)amewaaga wakazi wa mkoa wa Iringa kwa  kuchangia kiasi cha Tsh milioni 19 kwa ajili ya kutekeleza agizo la Rais Jakaya Kikwete la ujenzi wa maabara katika  shule za  sekondari.
 Dr Ishengoma akifungua moja kati ya  vikao  vya RCC Iringa kulia ni mkuu wa wilaya ya Iringa Dr Leticia Warioba 

Akizungumza katika mahojiano maalum na mtandao  wa www.matukiodaima.co.tz  leo , Dr Ishengoma  ambae ni mbunge wa  viti maalum mkoa wa Morogoro (CCM)  alisema  kuwa pamoja na  kutemwa katika nafasi hiyo ya  ukuu wa mkoa ila bado anampongeza sana Rais Profesa Jakaya  Kikwete kwa uteuzi  wake kama mkuu  wa mkoa nafasi   iliyoishi  mapema  mwezi  huu baada ya rais kuteua wakuu wa mikoa wapya  wanne na kufanya mabadiliko kwa maadhi ya  wakuu wa mikoa nchini na Iringa nafasi yake kuteuliwa Bi Amina Juma Masenza .

Dr  Ishengoma  alisema  kuwa kabla  ya  uteuzi  huo  alikuwa akiendelea na utekelezaji wa majukumu yake  mbali mbali ya  kupigania maendeleo ya  mkoa wa Iringa na kuwa  siku  moja kabla ya  uteuzi huo alianza  zoezi la kuhamasisa  ujenzi  wa  maabara kwa  kuanza kukabidhi  mabati  150 katika  Halmashauri  ya Manispaa ya Iringa zoezi ambalo alikusudia  kulifanya katika Halmashauri  zote na fedha hizo za kununua mabati kiasi cha Tsh milioni 19 amelazimika  kuzikabidhi kwa katibu tawala wa mkoa wa Iringa  ili  kuzikabidhi katika Halmashauri  zilizosalia ikiwmo ya  Iringa , Kilolo na Mufindi.
 
                                         Mkuu  wa  mkoa wa Iringa Dr Ishengoma wa tatu  kulia waliokaa akiwa na baadhi ya  wanahabari  mkoa  wa Iringa  na  viongozi wa wilaya ya Iringa na Manispaa ya Iringa katika moja kati ya vikao vyake na  wanahabari Iringa 
.............................................................................................................................................

" kila waka nilikuwa  nikiwasalimia kamwene ...makasi hii  ni kutokana na  wakazi wa mkoa   huu wa Iringa  kupenda  zaidi kazi .....niliupenda  sana mkoa  wa Iringa na  watu  wake  jinsi ambavyo  walivyo na moyo wa kujituma katika  kazi sitausahau  mkoa wa Iringa  na  nitaendelea  kuusemia vizuri mkoa  huu wenye  historia kubwa  nchini" alisema Dr Ishengoma

  DR  Ishengoma wa  pili  kulia   alipotembelea mabanda  ya wakulima  kuhamasisha  kilimo
.........................................................................................................................
Kuwa akiwa mkoani Iringa amehamasisha  ukuaji wa  sekta ya  utalii  mikoa ya nyanda za  juu  kusini hasa  mkoa wa Iringa kwa kuanzisha historia ya  chifu Mkwawa na utunzaji wa  kumbukumbu ya historia ya mkoa kwa  kushirikianana chuo kikuu cha Iringa .






0 comments:

Post a Comment

Design by Victor Simon -